Watu watatu wamefariki dunia kwa kunyongwa na miili yao kuchomwa moto ndani ya nyumba ya wageni iliyopo Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya.
Mauaji hayo yamegubikwa na utata kutokana na mazingira ya tukio hilo kuwahusisha wapangaji wa nyumba hiyo usiku wa kuamkia jana.
Mmiliki
 wa nyumba hiyo iliyopo Mtaa wa Kyela Kati, Boniface Mtengela alisema 
waliouawa ni watatu kati ya watu wanne waliofika kwa pamoja saa nne 
usiku jana.
Alisema watu hao walikuwa  wanaume watatu na mwanamke mmoja na waliouawa ni mwanamke na wanaume wawili.
Mtengela alisema wanaume wawili walijiandikisha kwa jina la Ali Hassan na mwanamke la Mariam. 
“Mwanamume mmoja alipanga chumba namba 14, mwingine 105 na mwenye mke alipanga chumba namba 15. 
"Waliokutwa wamekufa ni wanaume wawili wa vyumba na 14 na 105 pamoja na mwanamke huku mwanamume mwenye mke akitoroka,” alisema.
"Waliokutwa wamekufa ni wanaume wawili wa vyumba na 14 na 105 pamoja na mwanamke huku mwanamume mwenye mke akitoroka,” alisema.
Mganga
 Mfawidhi wa Wilaya ya Kyela, Francis Mhagama alisema uchunguzi wa miili
 ya marehemu hao umebaini kuwa waliuawa kwa kunyongwa kisha kuchomwa 
moto baada ya kumwagiwa mafuta ya taa.
Uchunguzi
 katika eneo la tukio ulibaini miili yao iliungua, lakini chumba na 
magodoro havikuungua. Ofisa Mtendaji wa Mtaa wa Kyela Kati, Timoth 
Luvanda alisema usiku wa tukio hilo hakusikika kelele zozote. 
Kamanda
 wa polisi mkoani Mbeya, Ahmed Msangi hakupatikana kuzungumzia tukio 
hilo wala kukamatwa kwa mmiliki wa nyumba hiyo na kuhojiwa katika Kituo 
cha Polisi Wilaya ya Kyela. 
Mhudumu
 wa nyumba hiyo, Hagai Yohana alisema mgeni mmojawapo aliondoka kabla ya
 saa 12 alfajiri akiwa na kidumu na mfuko wa rambo. 



 
 
 
 
 
 
1 comments:
Udta Punjab box office collection prediction release date star cast
ReplyUdta Punjab business report prediction
Udta Punjab Movie Reviews
Post a Comment