MNAMO MWAKA 2008 JOHN MNYIKA ALIANDIKA KATIKA MTANDAO WAKE HIVI "SERIKALI IACHE KUMLINDA LOWASA" LAKINI KITU CHA AJABU LEO HII WAMEMKARIBISHA MTU AMBAYE YE MWENYEWE ALIMWANDIKIA HUU WALAKA
Hebu usome hapa chini alivyo uandika mnyika kipindi hicho
Wednesday, September 3, 2008
SERIKALI IACHE KUMLINDA LOWASSA
Siku chache zilizopita. 
Nilitoa taarifa hii kwa vyombo vya habari. Hata hivyo, kwa sababu ambazo
 sizifahamu, habari hii haikutoka katika magazeti mengi ya kila siku. 
Pengine inaweza ikawa ni njia iliyotumika kufikisha ujumbe(barua pepe) 
lakini kuna uwezekano mkubwa sababu ikawa ni kuwa Lowassa hakutajwa 
kuchukuliwa hatua kama hizi ambazo nimezieleza hapa katika yale Maazimio
 23 ya Bunge. Yeye aliambiwa tu atakafakari na kuchukua maamuzi ambayo 
ataona yanafaa. Yeye akaamua kujiuzulu. Lakini bado siridhiki sana na 
sababu hii kwa kuwa maazimio hayo 23 hayajasema Karamagi na Msabaha 
wachunguzwe kuhusu Rushwa kama serikali ilivyoamua. Kama imeamualiwa na 
Serikali hawa wachunguzwe, kwanini serikali haikumjumuisha na Lowassa? 
Hii inafanya niamini kwamba bado msimamo huu hapa chini ni mwafaka:
TAARIFA KWA UMMA
SERIKALI IACHE KUMLINDA LOWASSA
- Ni mmoja wa mizizi ya ufisadi wa Richmond
- Akamatwe, ahojiwiwe na achukuliwe hatua za kisheria.
Tarehe
 25 Februari, 2008 Vijana wa CHADEMA tulitoa taarifa kwa umma tukikemea 
jitihada zilizokuwa zikiendelea za Lowassa kujisafisha na kusafishwa na 
tukahimiza achukuliwe hatua za haraka kutokana na tuhuma za ufisadi 
na/ama matumizi ya madaraka katika kashfa ya RICHMOND. Pamoja na taarifa
 yetu hiyo kwa umma katika kipindi chote ambacho Serikali ilipewa na 
Bunge kutekeleza maazimio ya Bunge kuhusu suala hilo hatua 
tulizopendekeza hazikuchuliwa. Aidha tumefadhaishwa zaidi na Taarifa 
ambayo Waziri Mkuu, Mheshimiwa Mizengo ameiwasilisha Bungeni Alhamisi 28
 Agosti, 2008 pamoja na kutaja hatua ambazo zimechukuliwa kuhusu 
watuhumiwa wengine ikiwemo kuandikiwa Barua za kujieleza na/ama kuanza 
kuchunguzwa na vyombo vya dola/usalama; Waziri Mkuu hakueleza hatua 
ambazo zimeaanza kuchukuliwa dhidi ya Bwana Lowassa. 
Tunatambua
 kuwa Waziri Mkuu katika taarifa yake ameeleza kuhusu hatua ambazo 
serikali imeanza kuchukua ikiwemo za marekebisho ya Sheria ama mifumo ya
 uwajibikaji, ikiwemo ile ya manunuzi. Hata hivyo, tungependa kuweka 
bayana kwamba matatizo ya msingi ya taifa letu hayasababishwi na 
mapungufu katika sheria pekee, ila kwa kiasi kikubwa yanasababishwa na 
kulegea kwa misingi ya utawala wa sheria na uwajibikaji miongoni mwa 
viongozi. Hivyo, tunapenda kuwajulisha Watanzania kuwa kama watuhumiwa 
wa ufisadi hawatachukuliwa hatua mapema, misingi ya utawala wa sheria 
itazidi kutetereka na matokeo yake ni kuwa mageuzi yoyote katika mifumo 
ya kiutawala hayatatekelezwa kikamilifu. Kwa ujumla tunaamini kwamba 
utamaduni huu wa kulindana katika serikali unatoa mfano mbaya kwa vijana
 wa kitanzania kuhusu uongozi na utawala bora.
Tungependa
 kusisitiza kuwa Bwana Lowassa, akiwa Waziri Mkuu wa nchi yetu wakati 
huo alikuwa mmoja wa mizizi mikuu ya ufisadi wa RICHMOND. Hivyo, tunaona
 kuwa Taarifa ya Utekelezaji ya Waziri Mkuu Pinda imejikita katika 
kushughulikia matokeo badala ya mzizi wa tatizo lenyewe na hivyo kama 
hali hii ikiendelea itaporomosha nidhamu na uwajibikaji katika taifa 
letu. Tunaamini kwamba kama Bwana Lowassa aliyekuwa kinara wa Serikali 
wakati huo, ataweza kuchukuliwa hatua kikamilifu basi itakuwa rahisi kwa
 waliokuwa chini yake kuweza kuchukuliwa hatua za haraka na hatimaye 
kurejesha maadili katika utawala. Lakini kama Serikali itaendelea 
kumlinda Bwana Lowassa na kuwatoa kafara maafisa wa chini, bado 
haitakuwa imetekeleza kikamilifu dhana ya uwajibikaji na utawala wa 
Sheria. Kujiuzulu kwa Waziri Mkuu na mawaziri wenzake kadhaa ni hatua 
ndogo sana katika kashfa iliyohusisha uvunjaji wa Sheria za nchi yetu, 
mazingira ya ufisadi na hasara kubwa kwa taifa.
Sisi
 tunaona kutotajwa kikamilifu kwa hatua zilizochuliwa juu ya Bwana 
Lowassa ni mwendelezo wajitihada za miezi ya karibuni za Bwana 
Lowassa(Mb) kupita akijitetea kuanzia katika hotuba yake alipokwenda 
Jimboni Monduli na kunukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari na hata 
mahojiano yake maalumu na Televeshioni ya Taifa(TVT).
Aidha,
 taarifa ya Waziri Mkuu Pinda imeakisi uamuzi wa Waziri Mkuu 
aliyejiuzulu Bwana Edward Lowassa kujitokeza miezi ya karibuni kujitetea
 kuhusu kuhusika kwake katika kashfa ya Richmond ambayo kwa ujumla ni 
ishara ya unafiki wa kisiasa. Itakumbukwa kuwa baada ya Kamati Teule 
kuwasilisha taarifa yake, Bwana Lowassa alipata nafasi bungeni takribani
 mara mbili kama kiongozi wa shughuli za serikali bungeni wakati akiwa 
Waziri kuzungumzia suala hili lakini hakutoa utetezi ambao Mwezi 
Februari alijaribu kuutoa kwa umma. Waziri Mkuu Pinda inabidi auleze 
Umma kama uamuzi wa kumtomtaja katika Taarifa yake ya utekelezaji kuhusu
 hatua ambazo amechuliwa ni ishara kuwa serikali imekubaliana na utetezi
 wa Bwana Lowassa.
Itakumbukwa
 kuwa Vijana wa CHADEMA tulieleza wazi kwamba katika kujitetea kwake 
mwezi Mei, Bwana Lowassa alithibitisha wazi uzembe na matumizi mabaya ya
 madaraka ambayo aliyafanya alipokuwa Waziri Mkuu wakati wa sakata zima 
la Richmond. Hivyo, tunarudia kutoa mwito kwa vyombo vya dola kuweza 
kumkamata, kumhoji na kumchukulia hatua za kisheria dhidi ya uzembe na 
matumizi hayo mabaya ya madaraka kwa mujibu wa sheria za nchi yetu. 
Badala ya Bwana Lowassa kuendelea kupita akijitetea kuwa Kamati Teule 
haikumuita kuweza kujieleza; vyombo vya dola vimkamate akatoe maelezo 
yake panapohusika. Vyombo vya dola vimekuwa vikiwakamata raia wa kawaida
 wenye taarifa za uhalifu kuweza kuisadia polisi, inashangaza Bwana 
Lowassa amejieleza wazi kuwa alikuwa anafahamu uhalifu uliokuwa 
ukitendeka lakini bado yuko nje akijitetea na pia Taarifa za kiserikali 
zikielekea kumlinda. Tunaamini akikamatwa yeye, atawezesha watuhumiwa 
wakuu wa kashfa ya Richmond kuweza kupatikana. Tulieza wazi katika tamko
 letu na Mwezi Februari kuwa , jitahada zozote za kumlinda na kumtetea 
zingeweza kuathiri mwekekeo wa hatua ambazo zitanatarajia kupendekezwa 
na Kamati ya Waziri Mkuu mpya Mheshimiwa Mizengo Pinda. Kutokana na 
Taarifa ya Waziri Mkuu Pinda aliyowasilisha Bungeni Alhamisi tarehe 28 
Agosti, 2008 ni wazi kuwa kuna kila dalili kuwa mwelekeo huo umeanza 
kuathiriwa, hivyo tunarudia tena kutaka Bwana Lowassa achukuliwe hatua 
kabla ya Bunge la Mwezi Novemba, 2008.
Bwana
 Lowassa akiwa Waziri Mkuu amethibitisha kwamba maneno yake mwenyewe 
kuwa alikiuka Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995 na 
Sheria ya Makosa ya Udhibiti wa Uhujumu wa Uchumi wa nchi ya Mwaka 1984.
Bwana
 Lowassa alikiri kwamba alikuwa anafahamu kwamba Richmond ni kampuni ya 
kitapeli, lakini katika kipindi chote cha uongozi wake aliinyamazia hali
 hii na kwa kiasi kikubwa aliitetea kampuni hiyo mbele ya macho ya umma.
 Wakati wa Viongozi mbalimbali wa upinzani walipoweka bayana kwamba 
Richmond ni kampuni isiyo na uwezo, serikali ilitetea kampuni hiyo. 
Vyombo mbalimbali vya habari vilimtuhumu Bwana Lowassa mwaka 2006 na 
2007 kama kiongozi wa Shughuli za serikali bungeni, kwamba alishiriki 
‘kuwaziba midomo’ wabunge wa CCM wasijadili suala hili. Pia, ni Bwana 
Lowassa huyo huyo, alinukuliwa akiwa Arusha akiwataka watanzania 
wasiijadili kampuni ya Richmond baada ya mvua kuanza kunyesha. Kama 
Bwana Lowassa wakati wote huo alijua kama ni kampuni ya kitapeli kama 
anavyojaribu alivyojaribu kujitetea, uamuzi wake wa kuwaasa watanzania 
wasiijadili ulikuwa ni wa kulinda ufisadi ambao aliufahamu. Inashangaza 
pia ni Lowassa huyo huyo alisema alijua kuwa Richmond ni kampuni ya 
kitapeli; ni Lowassa huyo huyo alisema kwamba alishauriwa vibaya na 
watumishi wa umma aliowataja kuhusu uwezo wa Richmond; Ni Lowassa huyo 
huyo aliyesema kwamba alijua kuwa TANESCO chini ya Menejimenti ya Net 
Group Solution walitaka kuhujumu mchakato wa tenda na hivyo 
‘kuwanyang’anya’. Lakini ni Lowassa huyo huyo aliyekuwa Waziri Mkuu 
ambaye angeweza kuviagiza vyombo vya dola kumwezesha kuthibitisha 
‘utapeli wa Richmond’; hivyo, maelezo ya sasa yanayotolewa kuhusu 
ushiriki wake yanaonyesha kuwa sasa kuna mwelekeo wa kumlinda.
Tunaendelea
 kushangazwa na Serikali na Bwana Lowassa kutumia utetezi wake kueleza 
tu nia yake ya kutaka mkataba wa Richmond usitishwe; nia ambayo kama ni 
kweli alikuwa na uwezo wa kuitekeleza na hakuitekeleza. Tunaitaka 
Serikali na Bwana Lowassa kuweka bayana ni kwa vipi Richmond ilipewa 
tenda hiyo na kwa shinikizo la nani. Bwana Lowassa anakwepa 
kuyazungumzia haya kwa kuwa anajua kabisa kwamba ni yeye aliyetumia 
madaraka yake vibaya alipokuwa Waziri Mkuu kwa kukiuka Sheria na 
Taratibu za Ununuzi kwa ‘kupora’ mchakato uliokuwa ukiendeshwa na 
TANESCO, ‘kuunda kamati yake’ na kuzisukuma mamlaka za ununuzi hali 
iliyopelekea Richmond kupewa tenda ili hali haikuwa na uwezo uliotakiwa.
 Ni uzembe huu ambao umelisababishia hasara taifa kwa kulipa shilingi 
milioni 152 kila siku  kwa kampuni ya Dowans 
iliyohamishiwa mkataba wa kitapeli wa Richmond; na takribani bilioni 172
 kwa ujumla ambazo taifa linawajibika kuzilipa kutokana na kukodisha 
mitambo hiyo.  Hvyo tunarudia tena rai yetu ya 
kutaka fedha zilizozilipwa kizembe mpaka sasa kurejesghwa serikalini. 
Kwa vyovyote vile, jitihada za Bwana Lowassa za kuhamasisha ujenzi wa 
Sekondari Kata, na utumishi wake kama Waziri Mkuu katika kipindi cha 
miaka miwili, haviwezi kuzidi hasara aliyosababisha katika uchumi wetu 
kipindi chote tulichokosa umeme wa dharura na wala hailingani na hasara 
ambayo tunaendelea kuilipa kila siku iendayo kwa Mungu. Maamuzi haya ya 
Bwana Lowassa yanaendelea kuwaumiza wananchi wote ikiwemo wa Jimbo lake 
la Monduli ambao wanataabika kwa mzigo wa gharama za umeme.
Tunarudia
 tena kumkumbusha Rais Kikwete kwamba Sheria ya Maadili ya Viongozi wa 
Umma inamtaka Rais kuhakikisha kwamba taratibu zinatengenezwa 
zitakazojenga maadili na kuongeza imani ya wananchi kwa uadilifu wa 
viongozi wa umma na katika taratibu za utoaji maamuzi ndani ya Serikali 
na katika sekta ya umma. Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma vile vile
 imeweka kanuni zinazotakiwa kuongoza utendaji wa viongozi wa umma: 
kwamba wanapokuwa madarakani, viongozi wa umma watakuwa waadilifu, wenye
 huruma, utulivu, umakini na watakaoendeleza viwango vya juu vya maadili
 ili kujenga na kuendeleza imani ya umma kwa uadilifu wa Serikali. 
Kuhusiana na utoaji wa maamuzi, viongozi wa umma watatekeleza wajibu wao
 kufuatana na sheria na kwa maslahi ya umma. Hivyo, taarifa ya Waziri 
Mkuu Pinda kutokueleza bayana hatua ambazo Bwana Lowassa ameshachukuliwa
 au atachukuliwa ni ishara kuwa kauli ya  Rais 
Kikwete aliyoitoa wakati akizungumza na Wazee wa CCM mkoani Dar es 
Salaam kwamba Bwana Lowassa amepata tu ‘ajali ya kisiasa’, na kumsifu 
kwa utumishi wake imechangia kumlinda mhusika huyu mkubwa katika sakata 
zima la RICHMOND. Vijana wa CHADEMA tulitarajia kuwa, baada ya Bwana 
Lowassa kukiri mwenyewe hadharani kuhusu uzembe wake na matumizi mabaya 
ya madaraka Rais Kikwete angelekeza hatua za kuchukuliwa dhidi yake 
badala ya kuendelea kumpamba kama “shujaa wa uwajibikaji’, kinyume na 
hayo tutaamini kwamba serikali yake inaendeshwa kwa ‘ubia wa kulindana’.
 Aidha tunarudia kutoa rai kwamba Rais Kikwete kuwafukuza kazi watumishi
 wote wa umma waandamizi ambao wametajwa na Bwana Lowassa kushiriki 
uzembe na matumizi mabaya ya madaraka; watumishi ambao walitajwa pia na 
Kamati Teule ya Bunge lakini mpaka sasa wanaendelea kutumikia nafasi zao
 mbalimbali. Kwa kuwa Waziri Mkuu Pinda ameshatangaza kwamba kwa wale 
wateule wa Rais, Kamati yake imeshapeleka suala zima kwake, tunategemea 
Rais atachukua hatua za haraka ili kuonyesha mfano kwa viongozi wengine 
wa chini yake wanaotarajiwa kuchukua hatua kwa watumishi wa chini.
Kadhalika
 tunapenda kuvikumbusha tena vyombo vya dola kwamba Sheria ya Udhibiti 
wa Makosa ya Kuhujumu Uchumi ya mwaka 1984 inatamka makosa yafuatayo 
kuwa baadhi ya makosa ya kuhujumu uchumi ni pamoja na yale yote yenye 
kusababisha hasara kwa mamlaka ya Serikali. Pia  Sheria
 ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11 ya mwaka 2007 inatamka kuwa 
ubadhirifu na/au ufujaji wa mali ya umma unaofanywa na watumishi wa umma
 na Matumizi mabaya ya madaraka kwa ajili ya manufaa binafsi, ni sehemu 
ya ufisadi. Bwana Lowassa alithibitisha kwamba maneno yake kwamba wapo 
viongozi waandamizi wa Serikali ambao amewataja kwa majina wamefanya 
maamuzi ya kifisadi, kitendo chake cha kunyamazia ufisadi huo- kinafanya
 iwe vigumu kwa yeye kutenganishwa na tuhuma za ufisadi zilizomo katika 
mchakato mzima wa kupewa tenda kwa kampuni ya Richmond na mambo yote 
yaliyotokea baada ya Mkataba huo kuhamishiwa kwa kampuni ya Dowans.
Aidha
 tumefadhaishwa na Taarifa ya Waziri Mkuu Pindi kwamba kujiuzulu kwa 
Waziri Mkuu na Baadhi ya Mawaziri ilikuwa ni ishara ya hatua ambazo 
serikali imechukua kutekeleza maazimio ya Bunge kuhusu suala husika. 
Tunarudia kukumbusha kwamba toka sakata la Richmond lilipoanza zaidi ya 
mwaka mmoja uliopita tulimtaka Bwana Lowassa kujiuzulu kulinda heshima 
yake lakini alikaidi na kuitetea kampuni ya Richmond. Uamuzi wa yeye 
kujiuzulu baada ya kashfa yote kuwa hadharani, umesaidia tu kuilinda 
serikali ya CCM lakini katu hauwezi kumpatia heshima ya uwajibikaji na 
wala hakuwezi kuwa ishara ya kwamba Maazimio ya Bunge yameshatekelezwa.
Kwa
 niaba ya Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA), kwa taarifa hii 
tunarudia kukemea jitihada zozote za kumlinda na kumtangaza Lowassa kuwa
 shujaa katika taifa letu kwani hali hii ikiachwa kuendelea inatoa mfano
 mbaya kwa vijana wa Tanzania. Tusingependa kwa namna yoyote katika 
taifa letu, mtuhumiwa wa ufisadi aliyetajwa pia katika orodha ya 
mafisadi(list of shame) kulindwa na kuenziwa kama shujaa wa Taifa letu 
kwani ni kuharibu maana nzima ya ushujaa katika uwajibikaji.
“Inasikitisha
 kwamba vijana wezi wadogo wadogo wakijazana magerezani. Vijana 
wamachinga kuendelea kukosa mitaji na maeneo ya kufanyia biashara; 
wanafunzi wa elimu ya juu wakipandishiwa ada na wengine kukosa mikopo- 
huku fedha za walipa kodi zikiendelea kuteketea kwa ufisadi na 
watuhumiwa wa ufisadi wakiendelea kutamba hadharani. Hali hii ikiachwa, 
itaharibu utawala wa sheria na kuleta matabaka katika taifa letu. Vijana
 tusingependa kuona nchi yetu inatumbukia kwenye migawanyiko kwa sababu 
ya kuwalinda watu wachache kwa kisingizio cha haki za binadamu”
Imetolewa tarehe 31 Agosti 2008 safirini Kenya na:
John Mnyika
Mkurugenzi wa Vijana
0754694553SOURCE - http://mnyika.blogspot.com/2008/09/serikali-iache-kumlinda-lowassa.html BONYEZA HAPO UONE VIDEO YA MTOTO MKALI; Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot.


 
 
 
 
 
 
1 comments:
hhizo kejeli,mwito kwamba nikamatwe vyote nimeviona na kwamba washirika wangu wa sasa ndio watuhumu wakuu,mm kama kiongozi wenu wa ukawa namuomba mungu anipe kura nyingi ktk uchaguzi mkuu,li baadae nije nichukue hatua mahsusu kwa wale wote waliohusika kinibatiza majina yasiosimilka vitabuni.mwenyezi mungu nisaidie.fisadi
ReplyPost a Comment