Boniphace Ngumije na Chande Abdallah
MASKINI mtoto huyu! 
Unapojaliwa kupata mtoto akiwa mzima asilimia 100 unatakiwa kumshukuru 
Mungu. Mwajuma Juma (25) mkazi wa Mbagala, Sabasaba Dar es Salaam, 
ameingia kwenye mtihani mzito tangu ajifungue mwanaye Yathib Rajab mwaka
 mmoja uliopita, akiwa hana sehemu ya kujisaidia haja kubwa.
Baada ya kugundulika kuwa 
na tatizo hilo madaktari wa Hospitali ya Taifa Muhimbili walimfanyia 
opasuaji na kumtoboa kwenye tumbo lake upande wa kulia na kuchomoa 
sehemu ya utumbo ambayo imekuwa ikitumika kumsaidia mtoto huyo 
kujisaidia.
Akizungumza na Ijumaa juzi,
 Mwajuma alisema kuwa madaktari walimwambia kuwa Aprili mwaka huu 
alitakiwa kurudi hospitalini hapo ili wamfanyie upasuaji wa 
kumtengenezea sehemu ya kutolea haja kubwa.
“Madaktari waliniambia 
utaratibu wa kuwasaidia bure watoto wenye tatizo hili umesogezwa mbele 
mpaka mwaka 2019. Ili sasa afanyiwe upasuaji zinahitajika shilingi 
1,350,000 ambazo sina kwani baba wa mtoto huyo alifariki dunia wakati 
nina mimba ya miezi sita.
Naomba msaada kwa Watanzania wenzangu ili mwanangu afanyiwe upasuaji, anateseka sana,” alisema mama huyo.


 
 
 
 
 
 
Post a Comment