BOFYA HAPA CHINI UONE VIDEO YA KIUTU UZIMA
Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa, amehitimisha ziara yake ya kutafuta
 wadhamini katika Mkoa wa Morogoro huku kada mkongwe wa Chama cha 
Mapinduzi (CCM), Kanali mstaafu Issack Mwisongo, akisema Baba wa Taifa 
hayati Mwalimu Julius Nyerere, hakuwahi kutamka kumkataa mbunge huyo wa 
Monduli kama ambavyo baadhi ya viongozi wanasema.
Katika Mkoa huo ambao ni wa 31, Lowassa alipata wanachama 104,038 waliomdhamini.
Kanali Mwisongo alisema tangu alipojiunga na Tanu mwaka 1967 ambayo sasa
 ni CCM, hajawahi kumsikia hayati Mwalimu Nyerere akitamka neno la namna
 hiyo na amekuwa akihudhuria vikao vyote kuanzia Halmashauri Kuu ya CCM 
(Nec), Kamati Kuu na Mkutano Mkuu.
“Mimi nimekuwa katika vikao hivyo vyote na kama Nyerere ukikosea au 
hakutaki, alikuwa anakukataa waziwazi na pia unatangazwa kwenye vyombo 
vya habari. Lowassa ni mtu anayewapenda Watanzania tangu zamani,” 
alisema Kanali Mwisongo.
Alitolea mfano wa mwekezaji aliyedai kuwa aliletwa na mmoja wa `wakubwa '
 ili ajenge hoteli katika chanzo cha gesi, lakini Lowassa aliyekuwa 
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa wakati huo, alikataa.
“Alikataza hoteli kujengwa katika chanzo cha gesi kwa manufaa ya 
Watanzania na kila alichoamua aliamua kwa manufaa ya Watanzania,” 
alisema Kanali Mwisongo.
Aidha, aliwaonya viongozi wa chama hicho kuacha kutoa matamshi kabla ya 
vikao havijakaa kwani ni makosa makubwa na wanasababisha CCM kuyumba 
kama hakina mwenyewe.
“CCM kimeyumba kupita kiasi kutokana na hawajui msemaji mkuu ni nani na 
vikao vikuu vinakaa saa ngapi vya kuamua hayo yanayosemwa ovyo. Viongozi
 wasifanye makosa katika Kamati Kuu, Kamati ya Maadili ambako kutakuwa 
na mizengwe, lakini watambue Nec ina nguvu,” alisema Kanali Mwisongo.
Naye Kada mwingine mkongwe, Dk. Juma Ngasongwa, ambaye amewahi kuwa 
Waziri katika awamu mbalimbali, alisema viongozi wa CCM wameyumba siku 
za karibuni kutokana na kusemana hadharani wenyewe kwa wenyewe  na 
Lowassa ndiye dawa ya kuondoa maneno hayo.
“Kuna wanachama wengi wamehamia vyama vingine kutokana na kushindwa 
kuongoza CCM. Sasa huko katika vyama vingine watawezaje kuviongoza? CCM 
irudishe wana-CCM imara madarakani ambaye ni Lowassa,” alisema Dk. 
Ngasongwa.
Kwa upande wake, aliyewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Steven 
Mashishanga, alisema vikao vinavyotarajiwa kukaa hivi karibuni 
vihakikishe vinatenda haki kwa kuangalia ni nani aliye na alama nyingi 
za vyema mgongoni na anayehitajika na wengi.
Alisema Lowassa ni kiongozi pekee mwenye uwezo na sifa za kuwa Rais kwani amekitumikia chama kwa miaka mingi.
Naye Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Morogoro Mjini, Fikiri Juma, alimtaka 
Nape Nnauye, kuacha kutoa kauli kuwa wananchi wengi wamepewa fedha kwa 
ajili ya kumdhamini Lowassa wakati wapo wagombea wengi wamefika kuomba 
udhamini na kutoa rushwa.
Alisema hakuna mtu aliyepewa fedha kwa ajili ya kumdhamini Lowassa, bali
 ni wananchi wenyewe ndiyo wana maamuzi ya mwisho ya kumchagua kiongozi 
wanayemtaka na si Nape.
“Haki isipotendeka katika vikao vya maamuzi sisi bado tupo pamoja na 
wewe, katika semina ya wenyeviti tuliyopewa tuliambiwa tuchague viongozi
 wanaokubalika ndani na nje ya Chama ambaye ni wewe,” alisema Juma.
Akizungumza na wanachama CCM, Lowassa aliwashukuru kwa kumdhamini na kwamba Mkoa wa Morogoro amepata watu wengi.
Hata hivyo, alisema licha ya kupata wadhamini wengi, atapeleka 
wanaotakiwa CCM na wengine atawahifadhi nyumbani kwake kama kumbukumbu 
yake.
Lowassa amepata jumla ya wadhamini 863,479 katika mikoa 31 aliyoitembelea.
Aidha, alitaja sababu za kugombea urais kuwa ni pamoja na kuchoshwa na 
hali ya umaskini na pia Rais Jakaya Kikwete, anamaliza muda wake wa 
uongozi hivyo anatakiwa kukabidhi kijiti kwa mtu mwingine.
"Na anayeweza kukipokea kijiti hicho na kuyaendeleza yale aliyoyaacha 
Rais Kikwete, ni mimi. Kazi hii haipatikani hivi hivi, naomba dua zenu 
Waislamu na Wakristo ni muhimu sana,” alisema Lowassa.
Alisema endapo atafanikiwa kupata nafasi anayoiomba, kwanza atahakikisha anafufua viwanda katika mji wa Morogoro.
Aidha, alisema anasononeshwa mno na migogoro ya wakulima na wafugaji kwa
 hiyo atakapoingia madarakani, ataunda tume ya kusuluhisha migogoro 
hiyo.
Aliwataka Watanzania wajiandae kuwa na `spidi' ya kuchapa kazi kwani 
anataka mchakamchaka wa Maendeleo na  atakayeshindwa atalazimika kukaa 
pembenBONYEZA HAPO UONE VIDEO YA MTOTO MKALI;
Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich.
Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology.
She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music.
She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot.
Loading...



 
 
 
 
 
 
Post a Comment